MFALME WA UVUMILIVU IMAM HASAN AL-MUJTABA (A.S.)

MFALME WA UVUMILIVU IMAM HASAN AL-MUJTABA (A.S.)

MFALME WA UVUMILIVU IMAM HASAN AL-MUJTABA (A.S.)

Publication year :

2007

Number of volumes :

1000

Publish number :

Toleo la Tatu

Publish location :

Dar es Salaam Tanzania

(0 Kura)

QRCode

(0 Kura)

MFALME WA UVUMILIVU IMAM HASAN AL-MUJTABA (A.S.)

Maisha ya mwanadamu yamejaa matukio ya kila namna ya kufurahisha na ya kuchukiza. Na sifa nzuri zaidi kwa roho ya mtu ni kuhisi kwamba yu alazimika kutimiza wajibu wake, na kiwango cha juu zaidi kwa heshima ya mtu ni kutimiza wajibu wake bila ya kujali gharama ya utimizaji wa wajibu huo. Ili kuijenga fikara hiyo katika akili zetu, ni lazima kujifunza maisha ya wale watu waliokuwa na madaraka katika mioyo yao na akili zao na ambao kila mara walifanya mambo huku wakiwa na fikara za kutimiza wajibu, ambazo hazikuingiliwa na maoni yao wala silika zao. Maisha ya familia ya Mtukufu Mtume (s.a.w.) yalikuwa ni mfano mzuri wa fikara za kiheshima na mtu kujiona kuwa yuna wajibu fulani. Tunaona maishani mwao aina mbali mbali za msingi huu muhimu sana. Kwa vile hali za maisha yao waliyokiishi hapa duniani zinatofautiana, kutoka mtu hadi mwingine, hali za maisha yao hutofautiana pia. Maisha ya mjukuu wa kwanza wa Mtume (s.a.w.), Imamu Hasan (a.s.) yalikuwa, peke yake, mfano wa uvumilivu, huruma, na ustahimilivu.